Collage aus Standbildern der Videoserie Unser Leben in Deutschland © Goethe-Institut

Yiğit, Riesta, Simone, Eric na Imam wamekuwa wakiishi Ujerumani kwa muda fulani. Wanaelezea maisha yao katika makazi  yao mapya. Kila mmoja wao ana hadithi tofauti.

Ujerumani , wanapitia mambo mengi ya kusisimua. Wakati mwingine wanapaswa kutatua hata matatizo madogo. Katika video unaweza kuona uzoefu wa vijana watano. Furahia.
 

Yiğit

Yiğit anatokea Uturuki. Anaishi Munich na anasoma huko. Yiğit anaishi katika bweni la wanafunzi. Pia ana mtu wa kubadilishana au kujifunza lugha. Mwenzake anataka kujifunza Kituruki na Yiğit anataka kuboresha Kijerumani chake.Kwa pamoja wanaweza kufanya mazoezi. Pia Yiğit huenda Stammtisch / meza au sehemu iliyoandaliwa kukutana na watu na kuzungumza Kijerumani.

Riesta

Huyo ni Riesta. Anatokea Indonesia. Sasa anaishi katika kijiji kidogo cha Berghausen. Anafanya kozi  shirikishi( ya lugha na mwongozo)  na anafanya kazi kama yaya katika familiya ya Kijerumani ambako anaishi. Katika muda wake wa ziada, huandika  kwenye blogu kuhusu uzoefu wake Ujerumani.

Simone

Simone anatokea Brazil. Ameolewa  na mtu wa Ujerumani na ana mtoto mdogo.  Familia hiyo  inaishi pamoja Möglingen. Hii ni sehemu ndogo. Simone anafanya kazi katika kampuni ya magari ya kijerumani. Humlea mtoto wake kwa lugha mbili. Baba huongea Kijerumani na mtoto na Simone huongea naye Kireno

Eric

Huyo ni Eric. Anatokea Kameruni na sasa anaishi Mannheim ambako anasoma pia. Eric anapenda kukaa na watu.  Ndiyo maana , anaishi kwenye ghorofa pamoja na wengine. Hupenda kupika na wenzake anaoishi nao  mapishi ya kimataifa na vyakula,  haswa vya Ujerumani, kama vile Kohlrouladen/ kabichi iliyochemshwa yenye nyama .

Imam

Imam ametokea Indonesia. Na anaishi katika mji mkuu wa Ujermani, Berlin. Huko anasoma na kufanya kazi. Imam ni mkufunzi katika kituo cha utamaduni wa Indonesia. Anawasaidia watu wa Indonesia kujifunza Kijerumani na kuwasimulia historia kuhusu Ujerumani. Katika muda wake wa ziada , hutembelea vivutio vya Berlin.